Pages

Wednesday 21 August 2013

SEPTEMBA MWAKA HUU USHOGA KUANZA KUFUNDISHWA SHULE ZA MSINGI UINGEREZA


Baada ya kupitisha sheria ya ndoa ya jinsia moja (same-sex marriage),huko nchini uingereza,
kutaanza kufundishwa somo la ushoga (gay marriage).
Somo hilo litaanza rasmi kufundishwa mwezi septemba mwaka huu kwa shule zote za serikali za primary.

watoto wa shule za msingi watakuwa wakifundishwa kuhusiana na masuala ya ushoga, usagaji, watu wa jinsia mbili, na watu wanaobadili jinsia (transexual), ili kuwafanya watoto hao kutambua makundi haya ya watu kama wenzao na kutowatenga.Shule za binafsi na za dini wana hiyari ya kuingiza katika mitaala yao ya ufundishaji somo hilo.

Tayari waziri wa Elimu wa uingereza Elizabeth Mary Truss maarufu kama Liz Truss,38 mbunge wa chama conservative ametoa onyo kali kwa walimu watakaokaidi kufundisha somo hilo kwa kufukuzwa kazi.Pia amewataka walimu hao kutangaza ushoga na usagaji kwani serikali itakuwa na mkakati wa kufanya kampeni ya kuwafanya watu wa 
makundi haya wakubalike kwa jamii. 

Miongoni mwa nchi barani ulaya zinazokubaliana na ndoa za jinsia moja ni pamoja na Sweden,ufaransa,Denmark,Norway,Uholanzi,
Iceland,Ureno,Ubelgiji na Spain.

Angalizo masheikh na wanazuoni wa kiislamu waanze kuitanabaisha jamii ya kiislamu kuhusiana na kasi ya jambo hilo la ndoa za ushoga,kwa kuweka mikakati maalumu ya uenezi wa mafundisho ya Mtume S.A.W

Baadhi ya kurasa za kitabu kitakachotumika kufundishia 

   



No comments:

Post a Comment