Pages

Monday 26 August 2013

BREAKING NEWS: SHEIKH MUHAMMAD BAKARI APATA AJALI DUMILA

Taarifa zilizopatika usiku huu ni kuwa mwanazuoni mkubwa wa ukanda huu wa Afrika mashariki sheikh  Muhammad Bakar Al burhan, Mudir wa madrasatil Shamsul maarif ya Tanga,amepata ajali maeneo ya dumila mkoa wa morogoro majira saa 8 mchana.

Ajali hiyo imesababisha majeraha kwa Sheikh Muhammad bakari katika maeneo ya kichwani,kifuani na mikononi.
Baadhi ya majeruhi wengine ni Mwalimu Mussa Kunema,Idd issa Nori na kambi salum.
Wengine waliokuwa katika msafara huo ni watoto wake Abdulhalim,Ahmad, Abuubakar pamoja na mkewe. 

Msafara huo ulikuwa unatokea Tanga kwenda kondoa kwa ajili ya kutangaza dini.
Majeruhi wote wamekwimbizwa katika hospitali kuu ya morogoro na wanaendelea na matibabu.
Aidha kuna taarifa zilizopatikana kwamba Mtoto wa Sheikh aitwaye Abuubakar amefariki katika ajali hiyo.Pamoja na mke mdogo wa sheikh bi ziyada naye amefariki.

Tunamwomba mwenyezi mungu amfanyie wepesi na kupona kwa haraka sheikh wetu na majeruhi wengine.
Aidha pia Mwenyezi mungu awasamehe na awafanyie wepesi marehemu wa ajali hiyo,aamin
Taarifa zaidi fuatilia blog yetu
Sheikh Muhammad Bakar Al burhan


kushoto ni marehemu Abuubakar  na ndugu yake ahmad

No comments:

Post a Comment