Pages

Tuesday 3 September 2013

CHUKI DHIDI YA UISLAMU: MSIKITI WAPAKAZWA DAMU YA NGURUWE

msikiti uliokuwepo katika jimbo la Quebec mji wa Saguenay kitongoji cha chicoutimi ,umepakazwa damu ya nguruwe na mtu asiyejulikana mwishoni mwa wiki iliyopita huko nchini Canada.

Tukio hilo limekuja wakati serikali ya jimbo la Quebec ikijiandaa kutangaza kupiga marufuku vazi la hijabu na vazi lolote lenye kuashiria dini katika sehemu zote za kazi.
Damu hiyo ya nguruwe imepakazwa karibu na mlango wa kuingilia katika msikiti huo pamoja na kuwekwa  barua inayowapa onyo waumini wa msikiti huo kuacha kujishughulisha na mambo yote ya dini yao Quebec au warudi makwao .

Aidha sehemu ya barua hiyo inasema  "msikiti huu umebatizwa kwa damu halisi ya nguruwe toka Quebec"
Chicoutimi ni moyo wa jimbo la Quebec ambapo inakadiriwa kuwa na wakazi 158,000, na silimia 99 ya wakazi wake ni watu wenye asili ya Quebec wanaoongea kifaransa  wa madhehebu ya katoliki.Asilimia iliyobaki ni waislamu na madhehebu mengine.Takwimu hiyo ni ya sensa ya mwaka 2011.

Akizungumzia tukio hilo meya wa mji Saguenay Jean Tremblay, amelaani kitendo hicho kwa kusema ni cha udhalilishaji na si cha kuungwa mkono na  pia hakiwakilishi mtazamo wa watu wa mji wake dhidi ya waislamu.

Aidha ametahadharisha endapo  serikali itawasilisha mezani muswada wa sheria wa upigwaji marufuku mavazi yenye uwashiria wa dini ili kuchunga tamaduni ya watu wa Quebec.Alisema kwamba mjadala kama huo utachochea chuki na matukio mbalimbali ya udhalilishaji dhidi ya uislamu.
“hakuna shaka kwamba uwasilishaji wa mawazo hayo dhidi ya kuukandamiza uislamu yataleta mtafukuru mkubwa.Kwa kutovaa alama yoyote ya kidini sambamba na hijabu kutainua hisia za wa Quebec kupinga dini ukilinganisha na hali ilivyo sasa,” aliongeza meya huyo wa mji wa Saguenay.

Wakati huo huo, wazalendo wahafidhina wanaiona serikali haikuchukua hatua za kutosha katika kudhibiti mchanganyiko wa tamaduni(dini na watu wasiokuwa wa Quebec) nyingine.
wahafidhina hao wa Quebec wanaiga mtindo wa kibaguzi  wakundi la kihafidhina la kimarekani lisilotaka waislamu nchini mwao.Suala la kuwapa hifadhi watu wachache wenye tamaduni tofauti na asili husika limekuwa likichemka kwa muda mrefu jimboni humo.

Watu wa jimbo hilo wamekuwa hawataki kuona utamaduni tofauti na wa kwao,ambapo mbali na kutaka kuwekwa sheria za kupiga marufuku vazi la hijabu,serikali ya jimbo hilo imekubali kupitisha matumizi ya lugha ya kifaransa kuwa lugha pekee itakayotumika jimboni humo.Mapendekezo hayo yameungwa mkono na wakazi wengi wa jimbo hilo.


Tukio hilo tayari limeripotiwa polisi, na wameanza uchunguzi wa kubaini nani aliyehusika.Mpaka sasa hakuna mtu yeyote au kikundi kilichodai kuhusika na tukio hilo.

Kwa mujibu wa mafundisho ya uislamu nyama na damu ya nguruwe ni haramu kwa ushahidi wa suratil Maidah aya ya tatu inayosema, "mmeharamishiwa mzoga na damu na nyama ya nguruwe....." 

Habari kwa hisani ya ahbaabur.blogspot.com

sehemu ya mbele ya msikiti iliyopakazwa damu ya Nguruwe

msikiti uliopakazwa damu ya nguruwe

No comments:

Post a Comment